Friday, October 30, 2015

Wajifunze kujiamini: Teach them to be confident

Habari wasomaji wangu,

Poleni na hongereni kwa mikiki mikiki ya uchaguzi.

Leo tuendelee na zile tips tulizoanza nazo wiki iliyopita:

Image result for raising a confident child
4. Praise them on small accomplishments. Mtoto anapofanya jambo jema hata liwe kidogo kiasi gani mtie moyo kwa kumpongeza, hii itampa hari ya kujaribu tena na tena

5. Allow them to choose their own path. Hii najua ni ngumu kuelewa ila ni muhimu kumzoesha mtoto kuchagua wenyewe njia wanayotaka kupita kwenye maisha. Tangu anapokuwa na kama miaka miwili mruhusu aamue nguo ya kuvaa n.k. Baba yetu hajawahi kutulazimisha kuwa watu fulani, amekuwa guardian tu, anaonyesha options tulizonazo na kuturuhusu kuamua

Image result for raising a confident child6. Ongea nao kuhusu strength zao na weakness zao. Hii itawasaidia kujua kuwa wana uwezo gani na wafanye bidii ya kuongeza yapi na kujifunza nini zaidi. Hii pia inasaidia watoto kuamua hata career (Kazi) zao za badae

7. Trust them. Jifunze kuwaamini watoto hata kama unapata shida kiasi gani. Wewe ndo mtu wa kwanza kuona jambo lao lolote na hivyo wanatamani uwaamini kuwa wataweza. Waruhusu kubeba glass na kadhalika


8. Have their back at all times, protect your own. Mimi huwa nashangaa mzazi anayeitwa shuleni na anasema, "Kweli huyu mtoto mjinga sana, hata nyumbani ni mzembe sana". Hii si sahihi, watoto wako wanategemea uwe upande wao, hata wanapokosea waonyeshe upendo na kuwasahihisha kwa upendo. Baba yangu na mama wamenichapa sana ila kila wakati najua wanaangalia my interest na hawawezi kuwa upande wa mtu mwingine zaidi yetu.

9.Allow them to be them not to be who you could not be. Baba yangu ni mwalimu, engineer na mama ni mwalimu ila hawajawahi kutushawishi kuwa wao, wametaka tuwe vile tunaona tunataka tuwe. Na tumefanya hivyo.

10. Give them a chance: Wape watoto nafasi ya kufanya mambo usitake kufanya kila kitu usiweke dada wa kazi wa kufanya kila kitu. Wape nafasi ya kujifunza kujitegemea


11. Give them constructive criticism. Jamani hii si kwa watoto tu ila hata kwetu. Inaumiza sana mtu anapokukosoa vibaya, ni vizuri kutumia nafasi hiyo kumweleza kuwa ni kwa jinsi gani angefanya vizuri zaidi. Nilipoingia form 1 nilikuwa wa 41 darasani kati ya watu 96, nikiwa shule ya msingi nilifeli mara moja nikawa wa tano (5), niliogopa sana. Ila baba aliniambia, " Agape ukijua kingereza vizuri utafanya vizuri sana".
Image result for raising a confident child
12. Learn to say SORRY. Najua kiafrika hii inakuwa nguvu, tunajiona kama vile sisi ni miungu na hatukosei watoto wetu. Ila sisi pia ni wanadamu na tunawakosea. Unapomuomba samahani anaona kuwa hata yeye anastahili heshima na ni mtu wa muhimu. Na hii itampa sana ujasiri na atajifunza kufanya hivyo kwa wengine.

13. Be their example of confidence: Jamani sisi ndo kioo cha watoto wetu, hawawezi kujifunza kama hawataona kwetu. Jiamini wewe na yeye itakuja kirahisi.

14. Show them that they are important by spending time with them. Jamani watoto wanaoingia kwenye makundi mabovu huwa hayo makundi yanawaonyesha kuwa wao ni wa muhimu na hivyo wanawabadili. Mpe mtoto muda wako aone yeye ni wa thamani sana na hii itamsaidia asisumbuliwe na mtu yeyote. Anajua anaye anayemthamini nyumbani.

All the best.
Image result for raising a confident child

ATM

Friday, October 23, 2015

Wafundishe kujiamini: Teach them to be confident

Habari za Ijumaa ya leo...

Naamini wiki imekuwa njema sana. Namshukuru Mungu kwa sababu anatutunza. Wiki hii mmoja wa wasomaji wangu wakubwa wa blog hii amepata baby boy. Many congratulation to them Hongera sana Nancy kwa kumpata your champion.


Image result for confident child
Nimekulia kwenye familia yenye baba ambaye ni muhubiri. Baadhi yenu mnaweza msielewe what it means kuzaliwa kwenye familia ya namna hii ila lets say all the complaints I had nikiwa mtoto well, nafurahi kuwa nilizaliwa huko. Anyway, baba yetu anatupenda sana na alikuwa anapenda kwenda na sisi kila anapokwenda, na sie jinsi tulivyokuwa tunapenda safari sasa yaani it was fun UNTIL tulipokuwa wakubwa enough kuweza kufanya utambulisho wenyewe.
Image result for confident child
Tulipofika umri wa kama miaka 13 hivi baba alitaka tujitambulishe wenyewe mbele ya watu badala ya yeye kututambulisha. Ilikuwa inaniogopesha mpaka siku zingine sitaki kwenda naye. Ila nikuambie tu hii imenipa sana confidence ya kusimama mbele ya watu. Haimaanishi kuwa huwa siogopi au sina wasiwasi lahasha imenisaidia kuona ni jambo linalowezekana na inanisaidia kuimprove kila wakati.


Sasa ni kwa jinsi gani unaweza kumsaidia mtoto kuwa confident? Au ni kwa jinsi gani baba yangu aliweza kutusaidia kuwa confident kuongea mbele ya mtu yeyote?

Hizi tips sio za kisayansi ni mbinu alizotumia baba yangu kwa watoto wanne (4) ambao so far tumeweza kwa kiasi fulani kuwa confident, siwezi kusema zinaweza kumsaidia kila mtoto kwasababu watoto wanatofautiana ila kwa ujumla unaweza kuchanganya na mengine na kufuatana na personality ya mtoto.

Tips:
1. Mruhusu mtoto wako kuwa na maoni nyumbani. Familia nyingi za kiafrika baba na mama na zingine baba tu ndo mwenye maamuzi yote nyumbani ila sio hivyo kwetu. Baba alitupa nafasi ya kusema kile tunaona kwenye mioyo yetu bila kutukaripia. Hii ilitufanya kuwa na ujasiri wa kuongea

2. Ruhusu watoto kuongoza mijadala nyumbani. Nimefikiria jinsi ya kuweka hii point. Nyumbani kwetu kila jioni kuna maombi na kila mtoto anasiku yake ya kuongoza in short unakuwa mchungaji wa siku hiyo, hii imetusaidia sio tu kuwa na ujasiri wa kuongoza mjadala ila uwezo wa analyse, kuchambua jambo...hii imetusaidia sana hata katika masomo yetu


3.Waonyeshe watoto kuwa kukosea ni sehemu ya kujifunza. Kwenye kujifunza kokote kuna kukosea kwingi na kama mzazi ni muhimu kuwa mvumilivu na kwa upole kabisa kumuonyesha mtoto njia nzuri ya kufanya jambo. Sikumbuki mimi kuchapwa kwasababu ya kuangusha glass...nakumbuka kuelekezwa cha kufanya nikiwa natumia glass.

Itaendelea...


Yours Truly,
ATM

Monday, October 12, 2015

Part 3:Loving your child can prevent them from becoming criminals: Kumpenda mtoto kwaweza kumuepusha kuwa mhalifu

Habari wapenzi wasomaji wangu,

Naamini ninyi na watoto wenu na familia ni wazima kabisa. Natamani nimalizie series hii ya muhimu sana.

Kwenye post yangu ya mwisho nilizungumzia kidogo kuhusu unyanyasaji na leo naomba nielezee halafu tumalizie. Mwaka huu unakaribia kuisha natamani tunapoanza mwaka mwingine tuweke malengo na mikakati mipya kuhusu malezi ya watoto wetu. Hilo nitalizungumzia wiki zijazo.

Tuendelee....


Image result for Child abuseAina za unyanyasaji/Types of child abuse
Kuna aina nne (4) za unyanyasaji wa watoto
  1. Sexual Abuse/ Unyanyasaji wa kingono
  2. Neglect/ Utelekezaji
  3. Emotional Abuse/Unyanyasaji wa kihisia
  4. Physical Abuse/Unyanyasaji wa kimwili
Sexual Abuse:
Any sexual activity, practice or instruction which either meets the criminal definition or is unhealthy for a child considering his/her age and level of development. Criminal activity is defined as “commit[ting] or allow[ing] to be committed any illegal sexual act upon a child including incest, rape, fondling, indecent exposure, prostitution, or allow[ing] a child to be used in any sexually explicit visual material.” - Haya ni matendo yoyote yanayohusiana na ngono, kumshika mtoto maeneo yake ya siri, kumpapasa, kufanya naye tendo la ndoa, kumuonyesha matendo ya ngono, au kuruhusu mtoto afanyiwe matendo haya na mtu mwingine. 

Vitendo hivi hufanyika sana majumbani mwetu bila ya wazazi kujua na mara nyingi watoto wanaogopa kusema. Hivyo ni muhimu kwa wazazi kuwa karibu sana na watoto wao ili wajue vitendo hivi. 

Muuaji mmoja anayeitwa Bobby Joe Long alisema yeye alilazimishwa kulala kitanda kimoja na mama yake mpaka akiwa na umri wa miaka 13 na alilazimika kuona mama yake akifanya mapenzi na wanaume...unaweza kugoogle
Image result for Child abuse
Neglect:
Is defined as failing or refusing to provide adequate food, clothing, shelter, emotional nurturing, or health care. It may also mean failing to provide adequate supervision in relation to the child’s age and level of development - Hii ni pale mzazi anapoacha kumpatia mtoto mahitaji yake ya msingi, chakula, malazi na mavazi, matibabu na ulinzi. Hii wengi wetu tunajitahidi kufanya ila wengine wanashindwa kufanya hasa kwa watoto wa kambo. Hii tunaiona sana kwa watoto wa mitaani na ni jambo la hatari sana hapo baadae kwa taifa

Carlton Gary huyu naye alikuwa muuaji anasema mama yake alikuwa anasahau kumpa chakula na hivyo alilazimika kula kwenye takataka

Emotional Abuse:
 Refers to any acts such as intentional humiliation, causing emotional conflict, or any act that could be psychologically damaging to the child, such as dressing a boy like a girl.Children that are subjected to emotional violence and humiliation by their parents or teachers, lack in self confidence and suffer from emotional problems during adulthood. These individuals caught in the cycle of violence could possibly become violent in adulthood.

Hii wazazi wengi hata wengine wetu tulifanyiwa na waalimu pia, kumtukana mtoto na kumdhalilisha, kumtembeza barabarani akiwa amefanya jambo kama kukojoa kitandani, ni hatari sana. Inaumiza watoto na kwa sababu hawezi kusema anaishia kuwa na kutojiamini na kuishia kuwa na maumivu na hasira inayoweza pelekea kuwa mhalifu
Image result for Child abuse
Physical Abuse:
 Is defined as causing or allowing any non accidental physical injury. 

Hii naomba nieleze kwa upole kabisa, wengi tumechapwa ila kuna wazazi wanaoumiza watoto kabisa eti wanawafundisha adabu. Ni muhimu kufahamu kuwa kumuadhibu mtoto kuna mipaka na sio kumuumiza. Ni muhimu kutokutoa adhabu ya kumchapa mtoto unapokuwa na hasira kali au unapokuwa na msongo wa mawazo. Ni muhimu kutulia na kutoa adhabu kwa umakini mkubwa sana.

Mbakaji na muuaji mmoja anaitwa Lorenzo Fayne yeye alikuwa anapigwa kichwani na mama yake.

Tafadhali share na sisi jambo lingine linalohusiana na unyanyasaji wa watoto.

Tafadhali wajulishe wengine kuhusu blog hii tuponye kizazi chetu.

Image result for Child abuse
ATM