Kabla sijafahamu kuwa ni mjamzito niliumwa kwa kama miezi miwil hivi na nilikunywa antibiotics kali sana. Zote zilikuwa zimeandikwa " Not to be used by women in their first trimester", yaani hazikupasa kutumiwa na wanawake wajawazito walioko kwenye miezi 3 ya kwanza.
Hapo ndo nilipoanza mawazo sana kuwa mtoto atakuwa kiziwi au kipofu au vipi. Daktari aliniambia nitajua matokeo nitakapojifungua. Iliniogopesha, niligundua kuwa siwezi kumwambia Mungu usinipe mtoto mlemavu...apewe nani sasa?
Niliyofanya:
- Nilimwambia Mungu mapenzi yake yatimizwe
- Nilimwomba Mungu anipe nguvu na upendo wa kulea mtoto hata kama atakuwa mlemavu
Happy parenting,
No comments:
Post a Comment