Monday, April 25, 2016

Movie: War Room, A must watch

Habari..

Nimekuwa busy na namshukuru Mungu kwa kunipa kuwa busy, wala silalamiki, ila sasa nimewamiss sana.

Sijapata muda wa kuwaletea mada zingine ila leo acha nikupe ushuhuda.
Image result for war room
Mimi nimejifunza kumuamini sana Mungu nikiwa na umri mdogo sana na Mungu hajawahi "kunilet" down hata siku moja. Haimaanishi sipiti magumu....On the contrary, Napita magumu mengi sanaaaa ila Mungu ni mwaminifu kabisa kunivusha.

Na kuna wakati namuuliza Mungu huwa ni kwa nini umeruhusu na hili, guess what na hayo pia anajibu. Kati ya mambo yanayoniweka busy sana sasa hivi ni project from Heaven ambayo Mungu amenipa as an answer to my prayer of WHY THIS LORD?

Najua hapo unaweza usielewe ila hiyo ni mada ya siku ingine na ukiona nimesahau kuileta please nikumbushe kabisa. Email yangu ni tunzo.agape@gmail.com na ukiwa na mada unataka tuizungumze tafadhali drop any comment there

So muujiza wangu mwingine wa very recent ni movie inaitwa War Room, Ok how is it a miracle naona unaweza usielewe ila jamani Mungu wetu ana njia nyingi sana za kujibu maombi yetu na mojawapo kwangu ilikuwa kupitia hii movie. Itafute na namuomba Mungu iwe muujiza kwako pia.

Watch the trailer here
https://www.youtube.com/watch?v=mIl-XY9t_Lw


Happy watching

ATM
Image result for war room
May God answer you when you PRAY

Monday, April 4, 2016

Kumuandaa mtoto wako kwa siku ya kwanza shuleni/Preparing your Child for the first day of school

Hello wasomaji wangu,

So my baby girl ameanza kwenda shule. Jamani yalikuwa maamuzi magumu ila inabidi aende. So ngoja nikupe tips nilizotumia na ambazo watu wengine wametumia sehemu mbalimbali duniani wakiwa wanawapeleka watoto wao shule kwa mara ya kwanza.

Image result for how to prepare your baby for school
1. Chagua shule nzuri.
Hili ni muhimu sana hasa mtoto anapokuwa hana umri mkubwa sana. So mimi nilifanya karesearch kadogo na nilitafuta sehemu ambayo mtoto hatakuwa anafanywa asome sana. Najua hapa wengi mtashangaa ila kwa umri wake sitaki sehemu ambayo atafanywa aweze kuhesabu mpaka 50 kwa miezi miwili....hapana. Nilitaka sehemu ambayo ni playful and fun..sehemu ambayo mtoto anakuwa mtoto. So mfano wa darasa la mtoto wangu wanakaa kwenye vigodoro like a camp, wanalala when tired and anatoka shule saa 6 mchana

2. Mueleze nini ategemee shuleni
Hapa usimwambie "Usiogope yote yatakuwa sawa" "Shule ni raha tu"..hapa ni uongo maana hata sisi wenyewe hatuamini hilo. Mueleze tu atakayoyakuta shuleni, wanafunzi wengi, waalimu kucheza kuimba. Ikiwezekana nenda katembelee darasa atakalosoma na yeye ili aone. Hii ni muhimu sana hasa kama mtoto amefikisha umri na hajawa na hamu ya kwenda shule.

3. Mkutanishe na watoto wengine
Image result for how to prepare your baby for school
Kama mtoto ni wa kwanza na hana majirani anaocheza nao basi ni muhimu kumsaidia kwa kumkutanisha na watoto wengine ili ajifunze social behaviors kama kushare vitu na kuishi na wenzake bila kuumizana. Mkutanishe na watoto wengine na mfundishe Dos and Don'ts.

4. Fikiria njia utakayotumia kuagana naye shuleni
Image result for how to prepare your baby for school
Ukimfikisha mtoto shuleni usimkimbie. Hii inamfanya mtoto aone kama hutarudi. Mueleze kuwa utarudi na hapo muage.
Mnaweza kuwa na goodbye kiss, Hi 5, a short prayer anything that works for you. Mueleze kuwa utarudi kumchukua au kama kuna mtu atamchukua basi mueleze.

5.Msomee mtoto wako
Image result for how to prepare your baby for school.
Hii nimeiandikia sana, kumsomea mtoto kunasaidia sana yeye kuwa na uelewa wa mambo haraka. Kusoma kuhusu umuhimu wa kumsomea mtoto kwako bonyeza HAPA.

6. Msaidie kukuza uwezo wake wa kusikiliza
Shuleni mtoto anategemewa kusikiliza na kufuata maelekezo mbalimbali hivyo ni muhimu mtoto kujifunza kufuata maelekezo mbalimbali.
Hata kama una dada wa kukusaidia kazi nyumbani ni vyema kumtuma mtoto vitu vidogo vidogo hapo nyumbani ili aweze kujua jinsi ya kufuata maelekezo.
Mwambie aondoe vyombo mezani. Mwambie apeleke viatu vyake sehemu ya kuweka viatu n.k.

7. Usilie unapomuacha shuleni hata kama analia
Image result for how to prepare your baby for school
Hii najua ni ngumu kumeza ila muonyeshe mtoto how strong you are na yeye atatulia. Ukilia na yeye atazidi kulia. Jikaze kalie badae. Hahahah...

8. Msaidie kukuza ubunifu wake
Image result for how to prepare your baby for school
Kabla ya mtoto kwenda shule ni muhimu kununua pencils, colors za aina mbalimbali, madftari...muache achore chore tu na kama ni mkubwa msaidie kufanya mazoezi kama kupaka rangi kuunganisha dots, kuunda maumbo na kadhalika. Hii inamsaidia motor skills hasa kujua jinsi ya kushika kalamu.

I wish you a great new beginning.

With love,
Image result for how to prepare your baby for school
Mama GG

Friday, March 18, 2016

Endometriosis, A silent struggle just got a voice

Have you ever had to write something with a lot a lot of emotions that you are shaken? Well this is me and I will tell you I will take up to 3 days to write this maana I need to compose myself to put this well.

Karibu.
Image result for millen magese endometriosis

Ok i have postponed this post kwa muda sasa ila ni wakati muafaka kuiweka. Nisameheni nitachanganya lugha sana

Endometriosis ni nini?
Ni hali inayotokea pale tishu zinazotakiwa kuota ndani ya kizazi (Endometrium) zinaota nje ya kizani na kuasababisha maumivu makali sana. Maumivu haya hutokea wakati wa hedhi, baada ya kufanya tendo la ndoa etc.

Ni nini dalili za Endometriosis?

  • Maumivu MAKALI kabla na wakati wa hedhi.
  • Maumivu sugu kwenye tumbo la chini na gongoni kwa chini
  • Maumivu wakati na baada ya tendo la ndoa
  • Kuona damu katikati ya mwezi kabla ya siku ya hedhi na kutokwa na damu nyingi sana wakati wa hedhi
  • Inasababisha pia kupata maumivu makali wakati wa kupata haja kubwa na ndogo
  • Baadhi ya watu wanakua na maumivu kiasi na wengine hushindwa kabisa kufanya kazi zao za kila siku.
  • Kushindwa kupata mtoto na wakati mwingine kunakuwa hakuna dalili kabisa

* Kuna watu wasiopata dalili kabisa

Nani anaweza kupata Endometriosis?
Mwanamke yeyote anaweza kupata Endometriosis, ila watu wengi wanajua hali yao wakiwa na miaka kama 30-40 hivi. Na uko kwenye hatari zaidi ya kupata shida hii kama, Hujawahi kupata mtoto, Hedhi yako hukaa kwa siku 7 au zaidi.
Image result for millen magese endometriosis
Utajuaje kuwa una Endometriosis?
Nenda hospital onana na daktari. Atakuuliza maswali kuhusiana na dalili na kucheck kama una makovu kwenye kizazi, "pelvic" na "cysts" . Wanaweza kukufanyia MRI au kukufanyia kitu kinaitwa "Laparoscopy", hiki kipimo kinafanyika kwa kuingiza kameraa kwenye tumbo kwa kufanya upasuaji mdogo, hii itaonyesha kama kuna vioteo vyovyote kwenye tumbo.

Je Endometriosis ina tiba?
Endometriosis haina tiba. Kama dalili ulizonazo si kali sana basi dawa za kutuliza maumivu zinatosha. Saa ingine doctor anaweza kukupa dawa za kusaidia homoni zako. Dawa zaweza kuwa za uzazi wa mpango ila hazitumiki kama unataka kupata mtoto baada ya muda mfupi.
Kama una maumivu makali sana basi inabidi operesheni ili kuondoa vimelea, vimelea hivi wakati mwingine hurudi pia. Kwa watu wengine ambao imekuwa kali sana basi hufikia hatua ya kutoa kizazi.

Kwanini nimeweka hii post wakati huu?
Pamoja na kushusha uwezo wa kufanya kazi kwa usanifu kwa wanawake wengi duniani kwa kuwasababisha walale vitandani na kushusha uchumi wao na familia Endometriosis inasababisha ugumba. Na hii kwa jamii zetu inasababisha maumivu sana kwa wanawake na kuvunjika kwa ndoa nyingi.

 Wengi tunamfahamu Millen Magese zamani alijulikana kama Happiness Magese. Huyu alikuwa Miss Tanzania na sasa ni mwana mitindo wa kimataifa. Yeye anaEndometriosis na ameamua kusema na kuwasaidia wasichana wengine walioko mashuleni ili wajue athari za hii hali.

Mwezi March ni mwezi wa kutoa habari "Awareness Month" ya Endometriosis. Ni muhimu sisi kama jamii kujua swala hili na kuwasaidia dada zetu, rafiki, mama,shangazi, wake zetu na watoto wetu wanaokua.

Kwa miaka mingi imekuwa ni aibu kwa wasichana kuongea mambo yao ya siri hadharani ila sasa inabidi liongelewe ili tupone. Na pia jamii iache mila potofu kuwa maumivu ni sawa tu, hapana, ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya zetu. Jamani tusiende tu hospitali mambo yakiwa very serios, tukiwahi hospitali msaada unaweza kutolewa na kuzuia athari zaidi.

This post is dedicated exclusively to Millen Magese, who fights Endometriosis on daily basis and who maintains a positive attitude and inspires million of people around the globe.

Asante sana dada Millen.

Unaweza kumfollow Millen Magese na Foundation yake kwa kufuata below links

Ladivamillen, MillenMageseFoundationEndometriosisAfrica, EndometriosisSwahili. Unaweza pata habari nyingi kuhusu Endometriosis kwenye Google.

Tazama video iliyotengenezwa na BBC wakati wa kampeni yake ya Africa Unsung Heroes iliyoonyesha clip ya Millen Magese. Bonyeza hapa

With Love,
ATM.