Wednesday, July 13, 2016

Jinsi sahihi ya kumlaza mtoto mchanga: Laying down your new born

Habari wapenzi wasomaji wangu.

Image result for how to lay down a newborn babyNaamini wote muwazima na mnaendelea vyema na shughuli zenu.

Mara nying tumekuwa tukisikia mtaani kuwa ukitaka mtoto alale vizuri mlaze kwa TUMBO. Hii imeaminiwa na watu wengi sana.

Mtoto mchanga HAPASWI kulazwa kwa tumbo wala kutumia mito. Mlaze mtoto kwa MGONGO. Hii inapunguza uwezekano wa mtoto kusuffocate (kukosa hewa).

"The American Academy of Pediatrics recommends that healthy infants be placed on their backs for sleep, as this is the safest position for an infant to sleep"

Mara nyingi tunasikia mtoto alikufa ghafla usingizini na tunabaki kushangaa kwanini. Mtoto mchanga ni rahisi sana kukosa hewa tofauti na mtu mzima. Akikosa hewa kidogo tu basi amefariki.
Image result for how to lay down a newborn babyJinsi ya kumsaidia mtoto kupata usingizi haraka:

  1. Hakikisha mtoto amekula akashiba
  2. Hakikisha ni mkavu, mbadili nepi kabla ya kulala
  3. Hakikisha mtoto amecheua. Hii inaondoa gesi tumboni inayosababisha mtoto kuumwa na tumbo. Baada ya kula kuwa na muda wa kutosha kumcheulisha mtoto.
  4. Wakati unambembeleza muimbie taratibu alale
  5. Ondoa vitu ambavyo vinaweza kumkosesha hewa mtoto kitandani. Mfunge vizuri na blanket au baby shawl. Weka midoli mbali na mtoto akiwa amelala
  6. Unaweza kumfanyia massage tumboni na miguuni taratibu akiwa analala
  7. Hakikisha mtoto hafunikwi sana akapata sana joto au akaachwa kufunikwa akasikia baridi
  8. Tumia muda wa mchana mwingi kucheza na mtoto ili alale zaidi usiku 
Unaweza soma zaidi mtandaoni

Wishing you happy parenting.
Yours,
ATM

Monday, June 27, 2016

ME TOO: MIMI PIA

Habari wapenzi wasomaji,

Naamini wote muwazima wa afya. Nimemiss kuwepo kwenye screen yako, na namshukuru Mungu kwa nafasi hii.

Image result for me too
Wengi wetu wakati tukiwa wadogo tulikuwa tukisikia wazazi ambavyo kila jambo unalofanya anakwambia yeye hakuwahi kufanya akiwa mdogo. Na kila mzazi alikuwa anakuwa wa kwanza shuleni. Ni watu wachache sana walioambia watoto wao kuwa shuleni alikuwa mtundu, mchokozi, alichapwa sana na alikuwa hafanyi vizuri sana darasani.

Hii haimaanishi kuwa wazazi wetu walikuwa wazazi wabaya, la, ilikuwa ni njia yao waliyoamini kuwa itatusaidia kuwa inspired kuwa kama wao. Ukweli ni kuwa njia hii si sahihi. Kwa sababu mtoto anaishi kwenye uongo na akijaribu sana kukufurahisha na kujiona ni mtu asiyeweza na kushangaa inakuwaje yeye ni mtoto wako na anafanya vibaya darasani au anaishia kukosa kila siku.

Image result for me tooHii inamjengea mtoto kutojiamini na kuwa mnyonge sana. Na pale atakapokuja kujua ukweli kuwa haukuwa kama ulivyomueleza, mara nyingi inamsababishia kutokukuamini tena na kuamua kuwa huru kufanya anavyojisikia.

Hii si kwa wazazi tu, ni jambo liko kwenye jamii, wahubiri na wachungaji, viongozi wa dini na makampuni hawapendi kuwaeleza watu "Failures" zao au mapungufu waliyokuwa nayo na jinsi walivyo yashinda na hii inatufanya kuwaona watakatifu na kujaribu kwa nguvu sana kuwa kama wao na saa ingine inatusababisha kujiona wabaya tusio na bahati, wajinga na wenye hasara sana.

Muhubiri mmoja alisema kuwa anapenda sana kumtumia mfalme Daudi anapowahubiria wanaume, Daudi ni mfano mzuri wa mambo wanaume wengi wanapitia na inakupa moyo kuona kuwa Mungu anasemehe na anakufanya mkuu.

Image result for me too
Kama wazazi ni vyema kuwa na tabia ya kushare challenges zako ulizopitia na mafundisho uliyopata ili kizazi chetu kipone. Tuwe wazazi wanaosema "ME TOO". Mfanye mtoto wako ajue ulivyo.

Do you struggle to be a perfect parent?- ME TOO
Do you feel you are not doing good enough for your children- ME TOO

I wish you a great week,
We are in this together
Image result for me too
Love,
ATM

Thursday, May 26, 2016

Agape's 5km Marathon

Habari za siku nyingi,

Naamini muwazima na mmeshapata nakala zenu za video ya War Room.

Image result for life is like a marathon
Wiki iliyopita nilipata bahati ya kushiriki marathon moja hivi na nikakimbia kilometa 5. Nilipoenda kama mita 200 nilikuwa nimechoka sikuwa na viatu sahihi vya kukimbilia,niliamua nitatembea badala ya kukimbia tu. Baba mmoja ambaye naye alishiriki alikuwa amechoka ila aliniambia mama twende. Kila akitangulia mbele yangu kidogo aliniambia jitahidi, twende etc. Na kila akisema hivi naongeza mbio au mwendo alifanya hivi mpaka nilipomaliza
Image result for life is like a marathon

Mbio zilifanyika barabarani kwa hiyo palikuwa na watu wanaoangalia. Kuna walioamua kunicheka tu bila sababu,wengine waliniambia kimbia dada unaweza tu. Wengine waliniambia siwezi chochote niache tu. Wengine walinitukana. Wengine waliniambie nipande baiskeli zao na pikipiki mpaka daladala. Wakati nakaribia kumaliza mbio mtu mmoja aliniambia wewe kwanza hata hujakimbia, ulikuwa umekaa tu mahali umejificha ndo umetoka ili umalize. Wewe huwezi kitu.

Wakati wa mbio mara nyingi nilitamani kuacha ila huyu baba ambaye na yeye alikuwa kwenye mbio hakuruhusu aliendelea tu kuniambia twende, fanya bidii. Usiache. Wakati wa mbio niligundua kuwa huyu baba hakuangalia nyuma kabisa, he kept going and looking forward, he was tired but he went and looked forward. Aliniambia, "Nawaangalia wale walioko mbele yetu, karibu tunawafikia". I doubted maneno yake ila we kept going.


Image result for life is like a marathon
Hii ilinifundisha somo kubwa sana kuhusu maisha. Life is like this marathon. Unafanya jambo ila kuna mambo mengi yapo njiani. Utakutana na watu wa aina nyingi kama hawa ambao nilikutana nao mimi. Wengine watakupa moyo, wengine watakukatisha tamaa wengine watakucheka, wengine watakutukana na kukudhihaki.

Cha muhimu kabisa ni PUT ON THE RIGHT SHOES, songa mbele. Never look back, look those who are before you. You went through a bad life experience, never look back look forward. In life keep moving, it does not matter how you move. Run, walk,crawl, just move. Mambo yanaweza kuwa magumu hakuna kukata tamaa, hairuhusiwi kukata tamaa, hakikisha unamaliza what you started.

Hata kwenye malezi ni hivyo hivyo. Kumbuka wewe ni mama au baba bora. Tia bidii. Omba, fanya kila kinachowezekana kufanyika kulea watoto vizuri. Hakuna mzazi perfect duniani. Tunakosea ila tunasahihisha tunasonga mbele tu.

Run your marathon well.
Image result for life is like a marathon

With love,
ATM